Kwa mujibu wa gazeti la Al Diyar la Lebanon, Jawad Nasrallah ,mwana wa kiume Sayyid Hassan Nasrallah amefichua mpango huo hivi karibuni.
Kwa mujibu wa mkanda wa video uliofichuka, kunatekelezwa njama ya kumuua Sayyid Nasrallah na kwamba njama hiyo inapangwa na mashirika ya kijasusi ya Saudi Arabia, Bahrain na ba baadhi ya nchi za Kiarabu katika Ghuba ya Uajemi zilivoshirikiana na mashirika ya kijasusi ya Mossad ya Israel na CIA ya Marekani.
Mzungumzaji katika mkanda huo wa video anasikika akisema kufuatia hotuba ya Sayyid Hassan Nasrallah baada kuuawa shahidi Sheikh Nimr, baadhi ya watawala wa eneo walikasirika na kughadhabika sana. Kwa msingi huo Shirika la Kijasusi la Saudia lilipokea amri kutoka kwa Mfalme wa Saudia kumuua Sayyid Nasrallah na kwamba jina la kiongozi huyo wa Hizbullah liwe katika orodha ya watu wanaopaswa kuuawa mara moja.
Katibu Mkuu wa Hizbullah manmo tarehe 3 Januari katika hotuba kwa njia ya televisheni alisema: "Kuawa Sheikh Nimr Baqir al Nimr , zaidi ya wakati wowote ule, kumeweka wazi kwa walimwengu uso wa utendaji jinai na ukufurishaji wa mfumo unaotawala Saudia."
Aidha Sayyid Nasrallah aliashiria njama na uwekezaji wa Saudia katika kuibua mifarakano katika ulimwengu wa Kiislamu na kusema: " Utawala wa Saudia unahusika katika kila sehemu panapo shuhudiwa mizozo baina ya Waislamu wa madhehebu ya Shia na Sunni."
Katibu Mkuu wa Hizbullah pia katika hotuba yake hiyo ambayo iliwakera sana watawala wa ukoo wa Aal Saud alibainisha kuwa: "Vitabu ya shule Saudia ndio vitabu ambavyo pia vinatumiwa katika shule za kundi la kigaidi la Daesh (ISIS).