Katika usiku huu washiriki waliosalia katika kitengo cha qiraa waliweza kusoma ambapo jopo la majaji lilitathmini qiraa hizo.
Washiriki katika kikao cha jana walikuwa ni kutoka Indonesia, Lebanon, Iraq, Egypt, Iran, Syria na Afghanistan ambapo walishiriki kwa njia ya intaneti kutokana na janga la corona.
Hivi sasa unaweza ukasikiliza klipu zilizo hapa chini za qiraa katika mashindano haya ya 37 ya kimataifa ya Qur'ani, na kisha uige sauti uipendayo katika qiraa hizo na baada ya kujirekodi tuma katika anuani ya @iqnanewsadmin kabla ya Machi 18.
Qiraa yako ya Qur'ani tukufu itawekwa katika tovuti ya IQNA na washindi watatangazwa Aprili 18.