Katika taarifa ya pamoja, taasisi hizo mbili muhimu za Kiislamu na Kikristo zimetoa wito kwa watu wote duniani kumuomba Mwenyezi Mungu aondoe janga la ugonjwa wa COVID-19 au corona na awasaidie wanasayansi kupata tiba ya ugonjwa huo.
Mnamo Februari 2019, Imam Mkuu wa Al Azhar Sheikh Ahmad el-Tayeb na Kiongozi wa Kanisa Katoliki Papa Francisi walitia saini waraka Waraka wa Urafiki wa Kibinadamu .
Wakati wa kuanza Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Papa Francis alimtumia salamu za kheria na fanaka Imam Mkuu wa Al Azhar na wawili hao walijadili pia njia za kuimarisha mshikamano wa dunia katika kukabiliana na janga la COVID-19.