IQNA

Mwezi wa Ramadhani

Dua za Kila Siku za Mwezi wa Ramadhani- Siku ya 12

Dua hizi za kila siku za Mwezi wa Ramadhani husomwa toka mwanzo ya tarehe mosi Ramadhani hadi siku ya mwisho katika mwezi huu mtukufu. Kila dua ina siku yake, na inaweza kusomwa mara nyingi kadiri ya uwezo wa mtu mwenyewe.

 

Ee Mwenyezi Mungu! Nipambe katika mwezi huu wa Ramadhani kwa sitara yaani (vazi) la kukuogopa, na Unisitiri katika mwezi huu kwa vazi la kukinai na kutosheka, na Unielekeze katika mwezi huu kwenye uadilifu na usawa. Na Unisalimishe katika mwezi huu na kila nikiogopacho kwa kinga yako Ewe Mhifadhi wa wenye kuogopa.

Habari zinazohusiana