Kwa mujibu wa taarifa Wazyauni hayo waliingia katika maeneo ya wazi ya msikiti huo na kutekeleza ibada za Kiyahudi huku wakidai kuwa eneo hilo linapaswa kujengwa kujengwa hekalu la Kiyahudi. Wapalestina waliokuwa hapo walikabiliana nao kwa amani huku wakitoa naraza la Allahu Akbar.
Katika miaka ya hivi karibuni, utawala wa Kizayuni wa Israel umeshadidisha hujuma na uvamizi wake dhidi ya maeneo ya Wapalestina ukifanya njama za kufikia malengo yake haramu katika ardhi za Wapalestina.
Msikiti wa al-Aqsa ambao ni kibla cha kwanza cha Waislamu umekuwa ukiandamwa na njama mtawalia za utawala vamizi wa Israel, hatua ambazo zinakwenda sambamba na ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika maeneo ya Wapalestina.